Breaking News
recent

MHE.WILLIUM LUKUVI ATAKA VIONGOZI WALIOHUSIKA KUBINAFSISHA SHAMBA LA HEKARI 3500 MOROGORO WAFIKISHWE MBELE YA SHERIA

Serikali imeliagiza jeshi la polisi na Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa kuwakamata, kuwahoji na kuwafikisha mahakamani viongozi na watendaji wote hata kama wamestaafu madaraka yao, walio husika kutoa shamba la ukubwa wa zaidi ya hekari 3,500, katika kijiji cha mlilingwa wilayani morogoro,.

Agizo hilo limetolewa na waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi, William Lukuvi ,baada ya kutembelea kijiji hicho cha Mlilingwa,Ngerengere, kwa lengo la kujiridhisha juu ya mwenendo mzima wa utoaji wa eneo hilo ambao ulitiliwa mashaka na rais.
        Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Willium Lukuvi akiongea na wananchi wa Kijiji cha Mlilingwa.
Mhe. Lukuvi amelazimika kukagua sahihi za wana kijiji walio orodheshwa majina yao ambapo wengi wa waliohojiwa wamezikana sahihi hizo na kueleza kushangazwa na hali hiyo na hata baadhi ya majina yaliyotumika ambayo sio ya wanakijiji wenzao na kudai katika kikao hicho hakuna mwenyekiti mjumbe wala mtendaji aliyekua kwenye sakata hilo aliyeudhuria kikao hicho.
   Wananchi wa Kijiji cha Mlilingwa wakimsikiliza waziri Lukuvi kwa umakini
Mwakilishi wa kampuni ya Oxfod TradingLTD aliyehudhuria mkutano huo wa kijiji, ameonekana kushindwa kujieleza vyema pale alipokuwa akihojiwa maswali kwa madai bado ni mgeni katika kampuni hiyo na hakuwepo wakati wa mkutano wa kuidhinisha kutolewa kwa eneo hilo,

Baada ya kujiridhisha, Waziri Lukuvi ameagiza mtu huyo kukamatwa na ofisa wa polisi ili kusaidia kukamatwa kwa wahusika wote wa sakata hilo na kuagiza uchunguzi pia kufanywa kwenye ofisi zote ili watakaobainika kuhusika na udanganyifu huo wafikishwe mahakamani


Waziri lukuvi amesema zoezi hilo litakua endelevu nchi nzima hivyo kutahadharisha kama kuna mwekezaji yeyote aliyejipatia ardhi kwa njia ya udanganyifu bila kufuata taratibu, ni vyema akaanza upya kufuata maagizo ya serikali,na ikibainika kuna kosa popote shamba lake litafutiwa milki yake na kubadilishwa matumizi kwa mujibu wa sheria.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.