Breaking News
recent

TUCTA YAITAKA SERIKALI KUPITA KIWANDA KWA KIWANDA,HOTEL KWA HOTEL KUANGALIA RAIA WA KIGENI WANAOFANYA KAZI BILA YA KUWA NA VIBALI MAALUM WANAOWAKOSESHA WATANZANIA AJIRA

Shirikisho la Wafanyakazi nchini Tanzania (TUCTA),limetiaka serikali kuongfeza juhudi katika upekuzi wa viwandani na sehemu nyinginezo za uzalishaji kwa kuwa wageni wengi wasio na vibali inasemakana wanafanya kazi huko.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jana Jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Shirikisho la Wafanyakazi, Nicolas Mgaya amesema wamebaini wageni wengi wanfanya kazi kwa kujificha katika viwanda mbalimbali nchini kwa kufanya kazi mchana na kutoka usiku.
             Katibu Mkuu wa Shirikisho la Wafanyakazi, Nicolas Mgaya 
Mgaya amesema ili fursa za ajira ziongezeke nchini srikali haina budi kupita kiwanda kwa kiwanda nyumba kwa nyumba ili kuwabaini wafanyakazi raia wa Kigeni wanaofanyakazi kinyume cha sheria.


Aidha Mgaya ameongeza kuwa kwa sekta nyingi za uzalishaji ikiwemo na mahoteli zimevamia na rais wa kigeni kutoka nchi jirani na kufanya shughuli ambazo hata watanzania wengine wa kawaida wana uwezo wa kuzifanya.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.