Breaking News
recent

PROF.IBRAHIM LIPUMBA AKANA KUHUSIKA NA VURUGU ZA KUVUNJIKA MKUTANO MKUU WA CHAMA CHAO ANASEMA ALIITWA NA WAJUMBE KUJIELEZA

Mwenyekiti wa zamani wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba amesema kuwa hausiki na vurugu zilizoibuka katika mkutano mkuu wa chama hicho uliovunjika juzi wakati wa uchaguzi wa kujaza nafasi zilizowazi.

Akitoa ufafanuzi huo jana Jijini Dar es Salaam, Prof. Lipumba amekiri ni kweli hakualikwa katika mkutano huo lakini aliombwa na baadhi ya wajumbe kwenda kutoa maelezo ya kwanini aliachia nafasi hiyo ya uenyekiti jambo ambalo viongozi waliokuwepo ukumbini hapo hawakulitaka.
   Mwenyekiti wa zamani wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba
Prof. Lipumba amesema kuwa anaheshimu maamuzi ya pande zote mbili kwa wanaomtaka arejee nafasi ya uenyekiti lakini pia maamuzi ya chama endapo utaratibu utafuatwa kwa kufuata katiba ya chama na demokrasia ya kweli ndani ya chama hicho.


Prof. Lipumba amekata kuhusika kukana kutumika na kisiasa na baadhi ya watu ili kukivuruga chama hicho na kusema kuwa viongozi wa chama hicho waepuke maneno ambayo yataweza kukigawanya chama hicho na badala yake wakijikite katika kudumisha demokrasia ndani ya chama hicho.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.