Breaking News
recent

Tanzania kusimamia Soko Huria Afrika Mashariki ili kuelekea kwenye uchumi wa kati bada ya miaka mitano

Serikali ya Tanzania imesema pamoja na kuzingatia amani inakuwepo katika nchi za Afrika Mashariki lakini pia itasimamia kupunguza makali ya Soko la Huria kwa nchi hizo ili kukuza uchumi wa Wananchi wake.

Akiongea na Waandishi wa Hbari Jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga amesema kupunguza makali hayo kutafanya kila mwananchi afaidike na Jumuiya hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga

Waziri Mahiga amesema kuwa kwa Mujibu wa Takwimu zinaonyesha kuwa Tanzania baada ya Miaka mitano ijayo itakua ni katika nchi zenye uchumi wa kati lakini kunatakiwa kuwepo uwiano wa Maisha katika ukuaji wa Uchumi huo.


Waziri Mahiga ameongeza kuwa pamoja na takwimu hizo kuonyesha hivyo lazima tanznia ifanye juhudi za makusudi kuwatoa wananchi wake kutoka pale walipo na kuelekea katika uchumi huo wa kati.


Aidha Dkt. Mahiga amesema katika kuingia katika soko hilo ni lazima nchi izingatie viwango bora vya bidhaa ambazo nchi itazalisha huku akisisitiza kuwa nchi itatoka kwenye kuuza malighafi na kuanza kuuza bidhaa zenyewe.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.