Breaking News
recent

Watumishi watano wa wa hospitali ya Butimba wilayani Nyamgana wasimamsihwa kazi kwa tuhuma za kusababisha vifo vya watoto mapacha

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza Baraka Konisaga amewasimamsiha kazi watumishi wa tano wa hospitali ya Butimba wilayani humo waliokua zamu ili kupisha uchunguzi wa tuhumza za kusababisha vifo vya watoto wawili mapacha vilivyotokea wakati mama watoto akijifungua.

Konisaga ametoa agizo hilo baada ya watoto hao kufariki dunia baada ya mama yao Suzan John Mkazi wa Jijini Mwanza kulazimika kujifungua kwenye beseni kufatia kukosa huduma baada ya wauguzi waliokua zamu kushindwa kumsaidia.
        Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza Baraka Konisaga
Akielezea tukio hilo mama wa Watoto hao marehemu Bi.Suzan John amesema kuwa baada ya kuzidiwa na kutaka huduma wauguzi wa waliokua zamu kila alipowaita walikua wanamuangalia na kuondoka na hali ilivyokua mbaya kwa msaada wa dada yake alilazimika kujifungua kwenye Beseni.

Mkasa huo ulisababisha hali ya Taharuki miongoni mwa Wananchi hususani wakinamama walioandamana hospitalini hapo na hivyo kulilazimu Jeshi la Polisi wilayani Nyamagana kuingilia kati huku wakina mama hao wakishusha lawama kwa watumishi wa Hospitali hiyo.

Baada ya Sakata hilo Mkuu wa Wilaya hiyo Bw. Baraka Konisaga alikutana na Uongozi wa Wilaya hiyo na kupata maelezo ya jinsi ya tukio lilivyotokea ndipo alipoamuru watumishi watano waliokuwa zamu kisimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi zaidi.

Watumishi waliosimamishwa kazi ni Wauguzi Suzana Singama, Bibi Ana Moshi, na Janeth Foya, pamoja na Madaktari wawili Maureen Magesa pamoja na Emiliana Mvungi.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.