Breaking News
recent

MFUMO MBOVU WA UWEKEZAJI BADO KIKWAZO KWA WAWEKEZAJI NCHINI KATIKA UMILIKI WA ARDHI

Wakati serikali ikihimiza suala la kilimo kwanza na uwekezaji katika sekta ya kilimo nchini kuweza kuwakwamua wananchi na umaskini, bado tatizo la mfumo wa upatikanaji wa ardhi limeendelea kulalamikiwa kuwa tatizo linalofanya jitihada hizo kukwama katika maeneo mbalimbali nchini hususani mkoani Lindi.

Hayo yamebanishwa na mwakilishi wa Mwekezaji kutoka nchini Ufaransa wa kampuni ya Cassava Starch of Tanzania Corporation LTD,.ambao wameshindwa kufanyia kazi azma yao ya kuanzisha kiwanda cha kutengeneza wanga katika eneo la Mtama, kitakachokwenda sambamba na ulimaji na ununuzi wa zao la mhogo ikiwemo kutoka kwa wakulima,kwa madai hali hiyo inasababishwa namlolongo mrefu wa mfumo wa upatikanaji wa ardhi,

Akitolea ufafanuzi suala hilo Mkuu wa mkoa wa Lindi Jordan Rugimbana ,amekiri mfumo uliopo kukwamisha hali hiyo ingawa maeneo mengi yapo wazi kwa shughuli za kilimo na uwekezaji, na kwamba kwa sasa ameanza kufanyia kazi hali hiyo kwa kuwatambua wawekezaji wote waliopo katika mkoa wake na kujua mahitaji yao na kile wanachofanya ambapo zoezi hilo la kuwapatia maeneo litawashirikisha wananchi.
              Mkuu wa mkoa wa Lindi Jordan Rugimbana 
Takwimu zinaonesha mkoa huo una eneo kubwa la ardhi ambalo linafaa kwa shughuli za kilimo lakini halitumiki,huku watafiti wakiwa tayari wamewawezesha kupata mbegu bora za aina mbalimbali kwa ajili ya kilimo cha mhogo.


Nao baadhi ya wananchi wa Mtama wilayani Lindi wameziomba mamlaka husika, kuhakikisha wawekezaji hao wanapata eneo la ukubwa wa hekta 6000 kama walivyoomba ili waanzishe kiwanda hicho cha kutengeneza wanga,na wao waweze kunufaika kiuchumi na fursa mbalimbali zikiwemo za ajira na maendeleo mengine.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.