Breaking News
recent

SAED KUBENEA APANDISHWA KIZIMBANI NA KUSOMEWA MSHTAKA YA KUMTUSI MKUU WA WILAYA YA KINONDONI

Mbunge wa jimbo la Ubungo na Mh. Said Kubenea leo amesomewa maelezeo ya awali ya tuhuma za kutumia lugha za matusi dhidi ya mkuu wa wilaya ya kinondoni Paul Makonda.

Akisoma maelezo hayo ya awali mbele ya hakimu mkazi mkuu, Thomas Simba wa mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam wakili wa serikali Mutalemwa Kisheni amesema kuwa mnamo tarehe14/12/2015 maeneo ya Mabibo Jijini Dar es salaam katika kiwanda cha Tooku Garmet co. ltd Said Kubenea alitoa lugha za matusi dhidi ya mkuu wa wilaya ya kinondoni wakati alipokwenda kuwasikiliza wafanyakazi wa kiwanda.
    Saed Kubenea (mwenye shati jeusi kulia), akizungumza jambo mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (mwenye t-shirt ya michirizi),

Hakimu Thomas Simba amehairisha kesi hiyo ya ambayo imefunguliwa kwa hati ya makosa ya jinai mpaka tarehe 20 na 21 January 2016 ambapo upande wa mashtaka wataanza kutoa ushahidi dhidi ya mtuhumiwa.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.