Breaking News
recent

Serikali yaombwa kuwachukulia hatua wanaofanya ukatili dhidi yao ikiwemo kuwakosesha elimu.

Kufuatia kukithiri kwa vitendo vya ukatili dhidi ya watoto ikiwemo kupigwa na kunyanyaswa na kunyimwa fursa ya kupata elimu ,baraza la Watoto wilaya ya Arusha limeiomba serikali ichukue hatua kali dhidi ya watakao bainika, ili kukomesha vitendo hivyo.

Hayo yameelezwa katika Baraza la watoto la wilaya ya Arusha lilokutana kujadili masuala mbalimbali ikiwemo haki za watoto ,Mjumbe wa Baraza hilo Hassan Kimaro amesema kuwa ili kuwa na taifa bora lenye ustawi ni vyema kukemea vitendo vya kikatili kwa watoto ili visigeuke desturi na kuathiri maendeleo ya taifa

Mwenyekiti wa Baraza hilo Dominic Raphael na Mjumbe wa Baraza hilo Brina Salvatory amesema kuwa kwa sasa wamejikita katika kutetea haki za hususan wale wanaofichwa majumbani na kuhakikisha kuwa wanafichuliwa ili waweze kupata haki zao za msingi ikiwemo elimu na mlo bora
       MWENYEKITI WA BARAZA LA WATOTO ARUSHA DOMINIC RAPHAEL
Mratibu wa wanawake na watoto jiji la Arusha ,Saumu Kweka amesema kuwa Baraza hilo la watoto limesaidia kufichua vitendo vya kikatili dhidi ya watoto na kuziwezesha mamlaka husika kuchukua hatua kali.

Changamoto inayowabili watoto nchini ni pamoja na matukio ya kikatili wanayofanyiwa majumbani ambayo asilmia kubwa hayaripotiwi katika vyombo vya sheria ,suala linalofanya ukatili wa kijinsia kukosa mwarobaini wa kisheria ambao unaweza kukomesha vitendo hivyo.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.