Breaking News
recent

TANGA YAANZA KUWASHUGHULIKIA WAHARIBIFU WA MAZINGIRA KUTOKA KENYA NA TANZANIA

Serikali mkoani Tanga imeanza kuchukua hatua za kudhibiti uharibifu wa mazingiza unaofanywa na wafanyabiashara.

Uharibifu huo unafanywa na wafanyabiashara wa Tanzania kwa kuashirikiana na wafanyabiashra kutoka Kenya kwa miti aina ya Mikarambati na Mikoko wilayani Mkinga.

Akiongelea uharibifu huo Afisa Misitu wa Wilaya hiyo Frank Chambo amesema miti ya mikoko imekuwa ikikatwa kwa ajili ya nishati huku Mikarambati ikitumiwa kwa ajili ya kuchonga vinyago na wafanyabiashara kutoka Kenya.


AKizungumza na ITV wilayani mkinga baada ya operesheni iliyofanywa awali kufanikiwa lakini baadhi ya wahamiaji kutoka nchi jirani ya kenya wameanza kuingia kupitia njia za majini na njia za panya Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama Mboni Mgaza amesema hatua hiyo inafuatia misitu ya hifadhi kuharibiwa vibaya katika baadhi ya maeneo na kupoteza uoto wa asili.
      Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama Mboni Mgaza
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.