Breaking News
recent

BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI(EALA),KUJITOSA RASMI KUSULUHISHA MGOGORO WA KISIASA NCHINI BURUNDI KUANZA KUCHUKUA MAONI YA WADAU

Bunge la Afrika Mashariki (EALA) sasa limeamua kujitosa rasmi kusuluhisha mgogoro wa kisiasa nchini Burundi, baada ya Asasi za kiraia na Taasisi mbalimbali zilizoko nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC), kuomba Bunge hilo kuingilia kati mgogoro huo na kuutatua.

Asasi na Taasisi hizo ziliandika maombi yao kwa Kamati ya Bunge hilo, inayoshughulikia migogoro na usuluhishi, ambao leo itaanza kusikiliza hadharani maombi yao, kwa siku tatu mfululizo na baadaye itapeleka mapendekezo katika Bunge hilo, kwa ajili ya kulitolitolea azimio

Akizungumza jana na waandishi wa habari jijini kwenye ofisi za Bunge hilo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Abdullah Ali Hassan Mwinyi amesema, wananchi wenye nafasi na kuguswa na suala hilo, wanakaribishwa kushiriki katika mhadhara huo, ambao utawasilisha maoni ya wananchi juu ya mgogoro huo wa Burundi.
Wabunge wa Tanzania kwenye bunge la Afrika Mashariki(EALA)wakitoka ndani ya ukumbi wa bunge hilo
Mwinyi amesema katika mhadhara huo, asasi hizo za kiraia na Taasisi zitawasilisha hoja mbalimbali za kulitaka Bunge hilo, kuingilia kati mgogoro huo na kwamba mapendekezo yatakayowasilishwa Bungeni, yatakuwa sehemu ya
mkakati wa kusuluhisha mgogoro huo.

Amesema wao kama Bunge wajibu wao kusikiliza pande zote, katika mgogoro huo
ikiwa ni pamoja na wananchi, vyama vya kiraia na kijamii,upinzani na hata
serikali, ili kuwa katika mazingira mazuri ya kuelewa kiini cha mgogoro na
kutoa mapendekezo stahili, yatakayomaliza mgogoro huo.

Amezitaja asasi hizo na baadhi ya Taasisi zilizowasilisha maombi kuwa
ni pamoja na Chama cha Wanasheria wa Afrika (PALU),Asasi ya Haki za Binadamu ya Attrocities Watch Afrika,Kituo cha Ushiriki wa wananchi wa Afrika katika Umoja wa Afrika,Chama cha Wanasheria wa Afrika Mashariki na Kituo cha Katiba.

Burundi imekuwa katika mgogoro wa kisiasa tangu Rais Pierre Nkurunziza
alipotangaza nia ya kuongeza muhula wa tatu wa uongozi wake mapema mwaka
jana, hatua iliyopingwa vikali na vyama vya upinzani nchini humo.

Licha ya kupingwa,Rais Nkurunzinza ameendelea na nia yake na kufanya
uchaguzi uliosusiwa na upinzani na kutangazwa kuwa mshindi huku mauaji ya
raia yakiendelea hasa baada ya jaribio la kumpindua kushindikana.

Mauaji hayo yamesababisha raia wengi wa nchi hiyo, kuikimbia nchi yao na
kusababisha mtafaruku wa mapambano kati ya majeshi ya serikali na waasi

ambao wamekuwa wakipambana katika mji mkuu wa Bujumbura nchini humo.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.