Breaking News
recent

HAKUNA ATAKELIPWA FIDIA KUTOKANA NA KUBOMOLEWA KWA MUJIBU WA SHERIA-SAID MECKY SADICK

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amesema watu waliojenga mabondeni wanaobomolewa nyumba zao hawatalipwa fidia ikiwemo kupewa viwanja na kuonya kuacha kuvamia mashamba ya watu kwa kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam Mkuu huyo wa Mkoa Bw, Meck Sadick amesema kuwa wakazi hao wa mambondeni wanapaswa kuondoka wenyewe wasibiri fidia ambayo haipo.
MWENYEKITI wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Dar es Salaam, ambaye pia ni Mkuu wa mkoa huo, Saidi Mecky Sadik
Meck Sadick amesema hayo huku zoezi la Bomoa bomoa likiwa linaendelea katika maeneo ya Mkwajuni huku akisisitiza kuwa zoezi hilo linafanywa kwa mujibu wa sheria ya mazingira ambayo inawataka wananchi wasijenge katika maeneo hatarishi.


Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amesisitiza kuwa zoezi hilo sio la Dar es Salaam peke yake kama wengi wanavyodhani bali ni la nchi nzima na litaendelea kwa kadiri siku zinavyokwenda.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.