Breaking News
recent

HAKUNA MTANZANIA ATAKAE KUFA KWA NJAA NCHI INA CHAKULA CHA KUTOSHA-KASSIM MAJALIWA

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassimu Majaliwa amesema kuwa hakuna Mtanzania atakayekufa kwa njaa kwa kuwa serikali ina akiba ya chakula cha kutosha kwenye maghala yake.

Aidha amesema kuwa kazi iliyopo hivi sasa kwa serikali ni ya kugawa na kupeleka chakula hicho kwenye maeneo yote yenye mahitaji ikiwemo maeneo yaliyokumbwa na mafuriko.

Waziri Mkuu ameyasema hayo alipofanya ziara ya kutembelea kijiji cha Majeleko kilichopo wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma ambacho ni miongoni mwa vijiji vilivyoathirika na njaa na kuwalazimu wananchi kuishi kwa kula matunda aina ya zambarau na baadhi ya wadudu.

Waziri Mkuu amesema bado kuna akiba nzuri ya chakula ambacho kitasambazwa maeneo yote yenye mahitaji nchini.


Aidha amewataka wananchi kuacha kutumia chakula cha msaada kwa ajili ya kupikia pombe na kila mmoja awe askari wa mwenzake na watakaobainika kufanya hivyo watachukuliwa hatua kali za kisheria. 
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.