Breaking News
recent

HALMASHAURI YA BAGAMOYO YAONGOZA NCHI NZIMA KWA UDANGANYIFU WA UUZWAJI NA UMILIKISHAJI WA ARDHI

Halmashauri ya Bagamoyo Mkoani Pwani inaongoza nchi nzima kwa udanganyifu wa uuzwaji wa ardhi kwa watu binafsi,kughushi Muhtsari ya majina pamoja na kutumia ardhi kukopea mabalioni ya fedha kwa maslahi binafsi.

Akizungumza na Watendaji wilayani Bagamoyo katika ziara yake ya kikazi waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amesema kuwa kuanzia sasa utaratibu wa uuzwaji wa ardhi ubadilishwe na kuwashirikisha wakuu wa wilaya.
       Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi
Mhe. Lukuvu ameongeza kuwa Wilaya hiyo inaongoza kwa kughushi kutokana na kuwa na mikutano mingi feki ikiwa ni pamoja na watu kuuziana Ardhi jijini Dar es Salaam na kupelekea copy tu za mikataba ambayo haijakidhi viwango vya uuzwaji.

Akiwa wilayani humo Mhe. Lukuvi alitembelea amsjara ya ardhi na kuvumbua madudu ikiwemo ucheweleshwaji wa hati za viwanja kwa watu wasiokuwa na kipato huku matajiri wakiharakishiwa huduma hiyo huku baadhi ya watendaji wakishindwa kutimiza wajibu wao.


Wakielezea matatizo wanayokutana nao vijijini hapo katika mkutano wao wake wa hadhara wananchi wengi wamesema kuwa wamekua wanadhurumiwa ardhi zao ikiwemo uuzwaji wa viwanja hivyo bila ridhaa yao huku wengine wakitishiwa.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.