Breaking News
recent

MAWAZIRI WAKUU WASTAAFU WALIOHAMA CHAMA WANA HAKI YA KUENDELEA KUHUDUMIWA NA SERIKALI KWA MUJIBU WA SHERIA NA KATIBA YA JAMHURI

Waziri wa nchi ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora Mhe. Anjela Kairuki amesema kuwa mawaziri wakuu wastaafu wanahaki yakuendelea kuhudumiwa na serikali kwa mujibu wa hitimisho la kazi namba 3 ya mwaka 1999 na kuendelea kupewa stahiki zao kwa mujibu wa sheria ya nchi inavyoelekeza.
    Waziri wa nchi ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora Mhe. Anjela Kairuki
Waziri Kairuki ameyasema hayo leo mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Dimani mhe. Hafidhi Ali Tahir ambaye alitaka ufafanuzi mawaziri wakuu wastaafu kujihusisha na siasa wakati huohuo bado wanahudumiwa na serikali na kuitaka sheria hiyo ifanyiwe marekebisho.

Waziri Kairuki amesema kuwa mawaziri wakuu wastafu wanahaki ya kujiunga na chama chochote au kujihusisha na masuala ya kisiasa kwakua ni haki yao kikatiba na haki hizo haziwezi kuingiliwa.


Wakati huohuo Waziri Kairuki amekemea tabia ya watumishi wa serikali ambao wanahudumia jamii kwa kubagua matabaka ya vyama kuwataka waache mara moja na watekeleze sera za serikali kwa kutambua kuwa nchi inamfumo wa vyama vingi.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.