Breaking News
recent

MCHUNGAJI CANNON KAJEMBE ATAKA POMBE YA VIROBA IPIGWE MARUFUKU KWA KUWA INACHANGIA VIJANA KUHARIBIKA

Vijana kote nchini wametakiwa kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya pamoja unywaji wa pombe uliopitiliza kwani unywaji huo unaathiri afya zao na kuteketeza nguvu kazi ya taifa pamoja na kuchochea maovu katika jamii ikiwemo,wizi,ubakaji na ukatili wa kijinsia.

Hayo yameelezwa na Mchungaji wa Kanisa la Anglican Church ,Cannon Kajembe katika ibada ya mazishi ya mtoto wa mtaani maarufu kama watoto wa dampo aliyefariki baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira kali kwa kuhusishwa na uporaji wa simu ya mkononi.

             Mchungaji wa Kanisa la Anglican Church ,Cannon Kajembe
Kajembe amewataka vijana kutumia nguvu zao kujenga jamii na taifa badala kujihusisha na matendo yasiyofaa huku akiitaka serikali iwachukulie hatua wauzaji wa pombe maarufu kama viroba .

Hata hivyo Mkurugenzi wa Kampuni ya madini ya Thom Gems,Thomas Munisi aliyejitokeza kusaidia ibada ya mazishi ya mtoto huyo wa mtaani ,amelitaka jeshi la polisi kuwachukulia hatua watu waliohusika na tukio hilo la mauaji kwani walijichukulia sheria mikononi hadi kutoa uhai wa kijana huyo ambaye mwili wake ulijeruhiwa vibaya kwa kipigo kikali hadi kifo.

Kwa upande wake Redman Joseph ambaye ni Mtoto wa mtaani na rafiki wa marehemu ameitaka jamii na serikali kuchukua hatua kuwasaidia watoto wa mitaani na kuwaendeleza ili kuepuka kujiingiza kwenye makundi mabaya ambayo huatarisha maisha yao na jamii kwa ujumla.


Mwili wa kijana Maiko Massawe aliefariki januari 22 umepumzishwa kwao maeneo ya Kibosho wilaya ya Moshi mkoa wa Kilimanjaro,Serikali,jamii na watu binafsi hawana budi kuwasaidia watoto wa mitaani ili kuokoa maisha yao na ndoto zinazopotea.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.