Breaking News
recent

MWALIMU ALALAMA KULAMBWA MAKOFI NA AFISA ELIMU KISA KUCHELEWA KATIKA DARASA LA SEMINA

Mwalimu wa shule ya Msingi Ikombohinga iliyopo wilayani Chamwino Mkoani Dodoma, Peter Hema, amechapwa makofi na Ofisa elimu wa hiyo Mohamed Msongo kwa kosa la kuchelewa kufika kwenye semina ya kufundisha watoto stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK).

Tukio hilo lilitokea baada ya mwalimu huyo kuchelewa kufika kwenye mafunzo hayo kwa takribani dakika 40 kwani alitakiwa kufika saa 2:00 lakini alifika saa 2:40 yeye pamoja na wenzake kwenye semina hiyo yenye lengo la kuwajengea watoto wa darasa la kwanza na la pili stadi za kusoma kuandika na kuhesabu.

Akielezea sakata hilo mwalimu alipigwa Peter Hema alisema kuwa Ofisa elimu huyo amemdhalilisha kwa kumpiga kibao baada ya kuchelewa kufika kwenye semina hiyo waliyokuwa wakiifanya.
       Waziri wa Elimu,Sayansi, Teknolojia na Ufundi Pro. Joyce Ndalichako
Kufuatia hali hiyo mwenyekiti Chama Cha walimu Wilaya ya Chamwino (CWT) Clementi Mahenga alisema kuwa chama hicho kinalaani vikali tukio hilo na kuitaka serikali kuhakikisha inamchukulia hatua kali za kisheria Ofisa elimu huyo kwa kukiuka kanuni na sheria za utumishi wa umma.

Alisema baadhi ya viongozi wamekuwa wakiitumia vibaya kaulimbiu ya Hapa kazi tu kwa kuwadhalilisha na kuwaonea watumishi wa ngazi za chini serikalini.

Alipotafutwa Ofisa elimu huyo ili kuzungumzia tuhuma hizo alikanusha vikali kuwa yeye hakumpiga vibao wala hakumsukuma mwalimu huyo.

Kwa upande wake Kaimu mkurugenzi wa Chamwino Richard Masimba alipotafutwa ofisini kwake alisema taarifa hizo hawana na watazifuatilia.


Masimba alisema ofisi haina taarifa ya mwalimu kupigwa vibao na kusukumwa ukutani na iwapo itathibitika hatua za kisheria na kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya Ofisa Elimu huyo.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.