Breaking News
recent

MWIGULU NCHEMBA AONDOA MIZIGO MINGINE VYAMA VYA USHIRIKA WA TUMBAKU IRINGA

Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvivu, Mwigulu Nchemba amewanusuru wanachama wa vyama vya ushirika wa kilimo cha Tumbaku wilayani Iringa kutapeliwa na baadhi ya viongozi wao, matrekta tisa yaliyokopeshwa kwa vyama hivyo kupitia mkopo uliotolewa na benki ya CRDB, miaka minne iliyopita.
          Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvivu, Mwigulu Nchemba
Ameamuru viongozi hao tisa kutoka chama cha ushirika Mfyome, Magubike, Kiwemu, Kitai, Mhanga na Kampuni ya umoja wa Wakulima wa Tumbaku Iringa (ITCOJE Ltd) wakabadhi ofisi zao mara bada ya kuondoka Iringa jana.

Pamoja na kuwataka viongozi hao waachie ngazi na taratibu za kujaza nafasi zao zifanywe haraka iwezekanavyo, Waziri Nchemba amemuagiza Mrajisi wa Vyama vya Ushirika nchini, Dk Audax Lutabazibwa kuifuta bodi ya ITCOJE na kuhakikisha taratibu za kuunda bodi mpya zinafanywa haraka iwezekanavyo.

Mbali na kumiliki gari la kisasa aina ya Toyota Land Cruiser VX bodi hiyo pia inamiliki roli aina ya Scania linalofanya kazi ya kusambaza kuni na pembejeo kwa wanachama wa vyama hivyo

Nchemba alikuwepo mjini Iringa juzi kwa mwaliko wa wakulima wa Tumbaku wa wilaya ya Iringa ambao pamoja na mambo mengi yanayohusu changamoto za kilimo na biashara ya tumbaku nchini, walimueleza jinsi baadhi ya viongozi wao wanavyotumia madaraka yao kujineemesha kinyemela kupitia mgongo wa vyama hivyo.

Kati ya watuhumiwa hao tisa yupo Mwenyekiti wa ITCOJE, Msafiri Pamagila na Afisa Ushirika wa Wilaya ya Iringa, Emanuel Samile ambaye waziri huyo ametaka achunguzwe kama alizingatia taratibu za kazi na sheria zinazounda vyama hivyo wakati naye akinufaika na moja ya matrekta hayo.

Kabla ya kutoa maamuzi hayo, Nchemba alitumia takribani saa 4 kuwasikiliza walalamikaji (wanachama wa vyama hivyo) na walalamikiwa (viongozi watuhumiwa) na kujiridhisha kwamba viongozi hao walitumia madaraka yao kufanya udanganyifu uliolenga kuwahalalishia umiliki wa matrekata hayo ambayo mkopo wake ulilipwa na wanachama wa vyama hivyo.

Akitumbua majipu, Nchemba aliyembatana na Lutabazibwa na Mkurugenzi wa Bodi ya Tumbaku Tanzania, Wilfred Mushi katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa siasa ni kilimo baina yake na wakulima wao alisema:

Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa na vyombo vyenu nitamke hapa hapa kwamba matrekta hayo ni mali ya vyama vya msingi, kwa kuwa yalikopeshwa kupitia vyama hivyo na yamelipwa na wanachama wenyewe kupitia vyama vyao vyao vya msingi kama ambavyo ushahidi kutoka CRDB unaonesha.

Mkurugenzi wa CRDB Iringa, Kisa Samwel alikiri katika kikao hicho kuvikopesha vyama hivyo mkopo uliotumika kununua matrekta hayo kwa kupitia mwavuli wao wa ITCOJE na wala mikopo hiyo haikuwa kwa ajili ya viongozi wanaotajwa.

Nikuhakikishie mheshimiwa waziri, benki yetu ilikopesha vyama na mikataba inaonesha hivyo; haya madai ya mikopo hiyo kugeukwa ya viongozi fulani hatuyafahamu na hayatuhusu. Kwetu sisi wakopaji ambao ni vyama ndio waliolipa mikopo hiyo na mpaka sasa nyaraka zinaonesha hivyo,” alisema.

Alisema mikopo ya matrekata hayo ilikwishalipwa na vyama hivyo lakini yameendelea kutumika kama dhamana katika benki hiyo baada ya vyama hivyo kuyatumia kukopa fedha kwa ajili ya msimu wa kilimo wa 2015/2016 unaonendelea.

Awali mmoja wa wanachama wa vyama hivyo, Ombeni Mvella alimwambia waziri kwamba inashangaza matrekata hayo ambayo mkopo wake ulilipwa na vyama hivyo, kumilikishwa kwa watu wachache kiunjaunja.

Mheshimiwa waziri tunanyanyaswa na viongozi wa ITCOJE, tulidhani ni watetezi wa wakulima, sasa wameguka kuwa wanyanyasaji wa vyama vya msingi,’. Matrekata yalikopeshwa na vyama lakini yemeguka kuwa mali ya viongozi wachache,” alisema.

Katika utetezi wao, watuhumiwa hao walisema waliteuliwa na wanachama wa vyama hivyo kuwa wasimamizi wa matrekta hayo kwa makubaliano kwamba watayamiliki moja kwa moja baada ya mikopo yake kwisha; jambo lililomshangaza waziri na viongozi wengine waliokuwepo.

Yaani kwa kuwa msimamizi tu basi mali husika inageuka kuwa yako. Kwahiyo na mimi nikisimamia wizara hii itakuwa sahihi kweli baada ya miaka mitano nipewe rachi moja au kingine chochote ambacho ni mali ya umma?” aliuliza kwa mshangao.

Akijitetea, Mwenyekiti wa ITCOJE alisema; “katika makubaliano yaliyotuwezesha kunufaika na matrekata haya hata sisi tulikuwa tukilipa fedha zetu. Mimi binafsi nililipa Sh Milioni 7 ili kupata trekta hilo ambalo pia nimekuwa nikilitumia kwa gharama zangu kulima mashamba ya wanachama wa vyama vya msingi.”

Naye Afisa Ushirika wa wilaya ya Iringa, Samile alijitetea akisema alipata trekta analomiki kwa kuwa yeye ni mmoja wa wanachama wa vyama hivyo vya ushirika mwenye mashamba makubwa.


Nikiri kwamba trekta langu nimelipata kwa kupitia mkataba wa kulisimamia kama ilivyo kwa wengine. Sijatoa hata senti tano katika mkopo wake na niseme wazi kwamba matrekta hayo yalikopeshwa kwa vyama vya msingi, sisi sio wakopaji wala walipaji; sisi tumepewa baada ya kuyasimamia,” alisema huku akitetemeka.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.