Breaking News
recent

SERIKALI YAANZA KUREJESHA ARDHI ISYOENDELEZWA NA WAWEKEZAJI KWA WANANCHI, YACHUKUA HEKTA 1800 ZA KIPUNGA ESTATE MBEYA

Serikali imeanza kurejesha ardhi kubwa ambayo baadhi ya watu waliimiliki kwa muda mrefu bila kuiendeleza huku wananchi wengi wakikosa ardhi kwa ajili ya kufanyia maendeleo.

Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi ametoa agizo la Hekta 1800 za Ardhi katika Shamba la Kapunga, Katika Kijiji cha Kapunga Wilayani mbalali Mkoani Mbeya zirejeshwe kwa Wananchi baada ya muwekezaji aliepewa ardhi hiyo kushindwa kuiendeleza.
         Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi 
Akiongea na Wanakijiji wa kijiji hicho katika Mkutano wa Hadhara Waziri Lukuvi amesema kwa rais alivyoagiza wakati wa kampeni zake kwa wale walioshindwa kuendeleza Ardhi na kushindwa kuiendeleza basi itarejeshwa kwa wananchi wa eneo husika kwa ajili ya kufanya Maendeleo.


Waziri Lukuvi baada ya kusikiliza kero za Wananchi wa Kijiji cha Kapinga amesema Rais Magufuli ameamua kuzirejsha kwa Wananchi hekta hizo 1800, baada ya mmiliki ya shamba la Kapunga Estate kumilikishwa kimakosa.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.