Breaking News
recent

TFDA YAJA NA MFUMO WA KUTATHMINI MAGONJWA YANAYOTOKANA NA ULAJI VYAKULA VISIVYO SALAMA

Mamlaka ya chakula na dawa nchini TFDA imeamua kuanzisha mfumo maalumu wa kutathmini magonjwa yanayotokana na ulaji wa vyakula visivyo salama na njia za kukabiliana na magonjwa hayo kwani vyakula hivyo vimetajwa kuchangia kwa kiasi kikubwa magonjwa yanayosumbua binaadamu.

Akiongea na kurasa Meneja mahusiano wa TFDA Gaudensia Simwanza amesema kuwa kwa muda mrefu sasa Tanzania inakabiliwa na changamoto ya kukosekana kwa takwimu sahihi na kwa wakati zinazohusu magonjwa yanayosababishwa na ulaji wa vyakula visivyosalama hivyo kuchelewesha kupatikana njia za kutatua matatizo hayo..
          Meneja mahusiano wa TFDA Gaudensia Simwanza
Akiyataja baadhi ya magonjwa yatokanayo na ulaji wa vyakula visivyo na ubora ni pamoja na kansa ya ini, magonjwa ya figo , magonjwa ya kuhara damu, homa ya matumbo, minyoo na amiba.

Aidha amewataka wanachi kuzingatia kanuni za afya wakati wa kuzalisha mazao ya chakula , uhifadhi wa chakula ,uaaandaaji wa chakula na ulaji wa vyakula kwani wakati mwingine chakula kinaweza kikazalishwa kwa kufuata kanuni za afya lakini vikahifadhiwa kwa madawa ambayo yanakemikali za sumu na hatari kwa afya ya binaadamu.



gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.