Breaking News
recent

TUMESHAFIKISHA FEDHA ZA ELIMU BURE KATIKA WILAYA ZOTE WAHUSIKA WAZIFIKISHE MASHULENI BILA KUCHELEWESHA-SIMBACHAWENE

Serikali imesema kuwa tayari imekwisha peleka fedha kwenye wilaya zote Tanzania bara na tayari wameshawapa wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi na kuwataka kuhakikisha wanazisimamia fedha hizo ziende moja kwa moja kwenye mashule husika bila ucheleweshwaji ili zianze kutumika.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa nchini TAMISEMI Mhe. George SimbaChawene leo Jijini Dar es Salaama alipoongea na East Afrika radio na kusema fedha hizo ni kwa ajili ya gharama walizokua wanatoa wazazi kwa shule za msingi na Sekondari nchini.
   Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa nchini TAMISEMI Mhe. George SimbaChawene
Simbachawene ameongeza kuwa fedha hizo zinatolewa kwenye mashule kulingana na idadi ya wananfunzi iliyonayo ikiwa ni pamoja na fedha za uendeshaji wa shule,fidia ya ada,fidia kwajili ya mitihani na chakula kwa ajili ya shule za bweni.
NEWS CLIP

Aidha Mhe. Simbachawene amekemea baadhi ya wakuu wa shule kuendelea kuwadai wazazi fedha kwa kisingizio cha wao kutoshirikishwa kwenye jambo hilo na kuwataka wazazi kuendelea kuchangia michango mbalimbali.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.