Breaking News
recent

WANASIASA WATAKA WIGO WA MAZUNGUMZO WA MGOGORO WA KISIASA KUPANULIWA YAWE ZAIDI YA VYAMA VIWILI IJUMUISHE NA TCD

Baadhi ya viongozi wa siasa nchini wametaka wigo wa mazungungumzo ya mgogoro wa kisiasa visiwani Zanzibari upanuliwe kwa kushirikisha wadau wote baada ya kuviachia vyama vinavyovutana vya CCM na CUF peke yao.

Akizungumza na Waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi Mhe. James Mbatia ametaka mgogoro huo kutatulia kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar pamoja na kuhusisha kituo cha demokrasia nchini ili kupata suluhusu ya suala hilo.
         Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi Mhe. James Mbatia
Mhe. Mbatia amesema kuwa mgogoro huo wa kikatiba usipotatuliwa na kuwafuata busara ya kuwahusisha wadau tofauti unaweza kusababisha machafuko visiwani humo na kuliharibia jina taifa pamoja na kugharimu maisha ya watanzania.


Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa chama cha sauti ya Umma (SAU),Bw. Yusuph Manyanga amesema kuwa majadiliano ya vyama viwili kwa sasa hayalengi kutafuta suluhisho kutokana na kila chama kuvutia upande wake.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.