Breaking News
recent

WHO KUITISHA MKUTANO MAALUMU KUJADILI KIRUSI CHA ZIKA KINACHOSEMEKANA KUATHIRI KINA MAMA WAJAWAZITO NA KUZAA WATOTO VICHWA VIDOGO

Shirika la Afya Duniani, WHO limesema kesho litaitisha mkutano maalum kuhusu kirusi aina ya Zika ambapo kirusi hicho tayari kimeripotiwa kwenye nchi 20 huku Brazil ikiwa ni nchi iliyoathirika zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo mjini Geneva, msemaji wa WHO Christian Lindmeier ameeleza kwamba kirusi chenyewe cha Zika si hatari, kwani huhasababisha tu ukurutu mwilini.
               Msemaji wa WHO Christian Lindmeier
Hata hivyo ameeleza kwamba Brazil imeshuhudia pia visa 4,000 vya watoto wanaozaliwa na vichwa vidogo, miongoni mwao 49 wakiwa wamefariki dunia, ikidaiwa hali hiyo kuwa na uhusiano na kirusi cha Zika.


Aidha amesema kwamba WHO haijapendekeza wanawake kujikinga dhidi ya kupata mimba, akieleza kwamba suluhu dhidi ya kirusi cha Zika hivi sasa ni kujikinga na mbu aina ya Aedes, ikiwa ni Brazil au kwingineko.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.