Breaking News
recent

11 WAFARIKI DUNIA NA WENGINE 29 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA GARI MKOANI TANGA HII LEO

Watu 11 wafariki dunia wakiwemo madereva wote wawili na mtoto mmoja wa umri wa miaka miwili na wengine 29 kujeruhiwa baada ya basi la abiria la Simba mtoto lilokuwa likitokea Jijini Tanga kuelekea jijini Dar es Salaam kupata ajali kwa kugongana na lori katika Mkoani Tanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Mihayo Msikhela amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa imetokea katika kijiji cha Pangamlima Barabara ya Tanga-Segera wilayani Muheza na kuongeza kuwa kati ya majeruhi wawili kati yao hali zao ni mbaya
     
Akielezea Chanzo cha Ajali hiyo Kamanda Mskhlea amesema kuwa ni uzembe wa Derva wa lori ajali ambae inasemekana alisinzia na kuhama upande wake na kuhamia upande mwingine wa barabara na kusababisha magari hayo kugongana uso kwa uso.

Kamanda Msikhela amesema kati ya watu walifariki dunia sita wamekwisha tambuliwa akiwemo mtoto wa miaka miwili huku akiongeza kati ya vifo Wanaume ni nane na wanawake ni watatu akiwemo na mtoto huyo wote wakiwa ni wa familia moja


gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.