Breaking News
recent

KIPINDUPINDU CHAENDELEA KUTIKISA NCHINI KWA WIKI MOJA CHAUA WATU TISA, SERIKALI YANG'AKA

Watu tisa wamepoteza maisha na wengine 473 wameugua ugonjwa wa kipindupindu katika kipindi cha wiki moja toka February 22 hadi 28 mwaka huu huku Mkoa wa mara ukitajwa kuongoza kwa maambukizi mapya ya Ugojwa huo.

Akiongea na Waandishi wa Habari jana Jijini Dar es Salaam Naibu Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Dkt. Khamis Kigwangala amesema licha ya jitihada za serikali kutokomeza ugonjwa huo lakini bado kuna baadhi ya wataalamu wa Afya pamoja na Wanajamii wanaendelea kuwa chanzo cha kuenea kwa ugonjwa huo.
 Naibu Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Dkt. Khamis Kigwangala
Mhe. Kingwala amesema wkumekuwepo na tabia ya Wataalamu hao wa Afya pamoja na Wanajamii kuficha wagonjwa pamoja na kutoa taarifa ya wagonjwa wachache kuliko uhalisia kunakwamisha juhudi za serikali kutokomeza ugonjwa huo.

Naibu Waziri huyo ametumia fursa hiyo kuzitaka mamlaka husika kutoka taarifa sahihi za wagonjwa ili kurahisisha njia za kupambana na ugonjwa huo ambao umeripotia karibu mikoa yote ya Nchini Tanzania.


Aidha amewataka viongozi wa Mikoa na Wilaya kuto kutoa kauli za kuwatisha wataalamu wa Afya na viongozi wa ngazi za chini kwa kigezo cha wagonjwa wa kipindupindu kwa ni kwa kufanya hivyo wataongeza kasi ya jamii kuwaficha wagonjwa wa kipindipindu.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.