Breaking News
recent

Kiwango cha umri wa kuishi kwa Watanzania kimeongezeka kutoka miaka 51 hadi miaka 61

Kiwango cha umri wa kuishi kwa Watanzania kimeongezeka kutoka miaka 51 hadi miaka 61 katika kipindi cha miaka kumi iliyopita sababu kuu ikiwa ni maboresho yaliyofanyika katika sekta ya afya nchini.

Naibu waziri wa afya Dkt Khamis Kigwangala, amesema hayo leo wakati wa uzinduzi wa matokeo ya utafiti wa kutathmini utoaji wa huduma za afya nchini, utafiti uliofanywa na ofisi ya taifa ya takwimu-NBS.

     Naibu waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Dkt Khamis Kigwangala
Kwa mujibu wa Dkt Kigwangala, mafanikio hayo katika sekta ya afya yameiwezesha nchi kuvuka kutoka katika kundi la nchi maskini na kuingia kwenye kundi la nchi za uchumi wa kati kwa upande wa sekta ya afya.

Naibu waziri Kigwangala ametaja maeneo yaliyofanikiwa kuwa ni katika upatikanaji wa huduma za uhakika za maji na nishati katika vituo vya tiba, huku maeneo mengi ya utoaji huduma za afya nchini yakiwa na wataalam wenye ujuzi unaohitajika katika maeneo yao ya kazi.


Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu ofisi ya Taifa ya Takwimu Dr Albina Chuwa amesema kuwa bado kuna changamoto ya wahudumu wa afya kupatiwa mafunzo ya ziada ili kuweza kukabiliana na vipimo mbalimbali na sera za afya zifanye kazi iliyotakiwa kwakutumia Takwimu mbalimbali nchini.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.