Breaking News
recent

MKUU WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM(UDSM),DKT.JAKAYA KIKWETE AMESEMA AMEPANGA KUBORESHA HUDUMA ZA ELIMU CHUONI HAPO

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete amemshurukuru raisi Magufuli kwa kumteua kuwa mkuu wa chuo na kuahidi kuendeleza upanuzi na uboreshaji wa chuo hicho.

Akizungumza na viongozi mbalimbali chuoni hapo baada ya kufanya ziara Dkt. Kikwete amesema atahakikisha chuo kikuu cha Dar es Salaam kinaendelea kuaanda wataalamu na viongozi na viongozi wa fani mbalimbali ndani na nje ya nchi.
       Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete
Dkt Kikwete alitembela vitivo mbalimbali katika chuo hicho kwa ajili ya tafiti na maktaba zitakazowezesha chuo hicho kupokea wanafunzi wengi zaidi ambapo kwa sasa chuo hicho kinapokea wanafunzi 22,000.

Rais Kikwete amesema anatamani chuo hicho kiwe chuo kikubwa nchini na Afrika kinachotoa viongozi ambapo mtu akitaka mtaalamu yoyote aweze kufikilia kwanza muhitimu wa chuo kikuu kabla ya kufikiria kwengine.


Kwa upande wake Makamu Mkuu wa chuo hicho Pro. Rweikaza Mukandala amemshukuru rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kumteua Dkt. Kikwete kuwa mkuu wa chuo hicho kutokana na mchango wake katika chuo wakati yupo madarakani.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.