Breaking News
recent

TANZANIA IMESEMA HAINA MPANGO WA KUJITOA KATIKA MAHAKAMA YA KIMATAIFA YA ICC

Tanzania imesema haina mpango wa kujitoa katika mahakama ya kimataifa ya ICC na kutaka kufanyiwa marekebisho ya baadhi ya vipengele vinavyolalamikiwa kuwa haitendi haki na imekuwa ikiwaonea viongozi wa bara Afrika.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu siku miamoja na serikali ya tano, waziri wa mambo ya nje, ushirikiano wa Afrika Mashariki wa kikanda na kimataifa balozi Agustine Mahiga amesema ushindi wa rais wa Kenya na Bwana Uhuru Kenyata na makamu wake William Ruto umedhihirisha kuwa waafrika wanaweza kuishinda mahakama hiyo, na kusisitiza kuwa baadhi ya vipengele vilivyowekwa lazima vitazamwe upya.
  Waziri wa mambo ya nje, ushirikiano wa Afrika Mashariki wa kikanda na kimataifa balozi Agustine Mahiga 
Aidha akizungumzia siku 100 za serikali ya awamu ya tano, Balozi Mahiga amesema mafanikio mengi yamepatikana katika kuimarisha siasa za kimataifa ikiwemo kuleta maridhiano katika kulijadili mgogro wa Burundi, kuitangaza Tanzania kimataifa pamoja na kuweka wazi misiamo ya Tanzania iliyosaidia kuwa na nguvu ya pamoja na nchi marafiki katika kutatua changamoto zilizopo nchni.


Aidha Balozi Mahiga amesema rais Dkt John Pombe Magufuli anatarajiwa kuhudhuria mkutano wa kimatifa wa marais wa nchi za Afrika Mashairiki unaotarajiwa kufanyika mapema mwishoni mwa mwezi huu mjini Arusha, ambapo Tanzania ni mwenyekiti wa mkutano huo unaolenga kujadili swala la kudumisha ushirikiano ndani ya nchi wanachama na changamoto zinazojitokeza.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.