Breaking News
recent

WACHINA 13 WASHIKILIWA WILAYA GEITA KWA KUFANYA SHUGHULI ZA UCHIMBAJI MADINI BILA YA KUWA NA KIBALI MAALUMU CHA KUFANYIKA KAZI NCHINI

Idara ya uhamiaji mkoani Geita inawashikilia raia 13 wa China kwa tuhuma za kufanya kazi za kutafiti pamoja na kufanya kazi za kuchenjua madini ya dhahabu kinyume cha sheria.

Watuhumiwa hao wamekamatwa katika machimbo ya Igo katika kijiji cha Nyamahuna wilayani Geita kufatia msako mkali kwa wageni wa mataifa kutoka nje wanaofanya kazi Mkoani humo bila ya kuwa na kibali.
        Raia wa china wakiwa Migodini Nkasi wakiwaendelea kufaya kazi
Akizungumza mara baada ya kuwakata watuhumiwa hao Afisa Uhamiaji mkoa huo Charles Washima amesema watuhumiwa hao waliingia nchini kwa kibali cha matembezi lakini wamekua wakijihusisha na ufanyaji kazi kinyume na Sheria.


Nae Mmiliki wa Mgodi huo Bi. Rehema Abdallah alishikiliwa na Idara hiyo baada ya kuhusika na kuwaleta raia hao wachina kufanyakazi katika mgodi wake bila ya kuwa na kibali maamulu.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.