Breaking News
recent

WASIOWEZA KUFANYA KAZI NDANI YA WIZARA YA UJENZI,NA UCHUKUZU WATUACHIE OFISI KABLA YA KUTUMBULIWA-PROF MBARAWA

Waziri wa Ujenzi ,Mawasiliano na Uchukuzi profesa Makame Mbarawa amewataka wafanyakazi wote wa wizara yake mkoani simiyu kuwa waadilifu na atakayeshindwa kufanya hivyo ataonyeshwa mlango wa kutokea kwa kupewa kilichochake ili kupisha wanaohitaji kufanya .

Kauli hiyo ameitoa wakati wa ziara yake ya siku moja mkoani simiyu ya kukagua barabara ya Lamadi hadi Bariadi yenye kilomita 71 ambayo iko katika hatua za mwisho kukamilika na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami mwigumbi Shinyanga hadi Maswa yenye kilomita 50.3 pindi alipokutana na wafanyakazi wote walioko katika wizara yake
           Waziri wa Ujenzi ,Mawasiliano na Uchukuzi profesa Makame Mbarawa
Waziri amesema kuwa uadilifu katika sekta ya miundombinu ni muhimu katika kuchochea kasi ya maendeleo na hatimaye Tanzania kuingia katika uchumi wa kati ,hivyo ni vema wafanye kazi kwa bidii na ubunifu sambamba na kujiepusha na vitendo vya rushwa.

Akiwa katika kambi ya kampuni ya chicco inayojenga barabara ya mwigumbi maswa amemtaka mkandarasi kufanya kazi ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha kizuri na akifanya kwa kiwango cha chini hatasita kumuondoa na kumtafuta mkandarasi mwingine.


Aidha alitoa onyo kwa wafanyakazi wa sekta ya mawasiliano kutojihusisha kuwa madalali wa makampuni mengine, huku akitolea mfano kampuni ya TTCL na endapo akisikia mtu anajihusisha na hilo lazima atamuondoa kazini.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.