Breaking News
recent

Watu 3 wanaodhaniwa kujihusisha na matukio ya kigaidi wameuwawa jana katika eneo la sinoni Engosheraton mkoani Arusha

Watu 3 wanaodhaniwa kujihusisha na matukio ya kigaidi wameuwawa jana katika eneo la sinoni Engosheraton mkoani Arusha baada ya kutokea majibizano ya silaha na Polisi waliofika eneo la tukio kwaajili ya kuwakamata watu hao.

Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi Mkoani Arusha kati ya watu hao ni mmoja pekee ambaye ametambuliwa kwa majina ya Athumani Ramadhan Kassim mwenye umri wa miaka 26 ambaye ni mzaliwa wa Mkoani Tanga

Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha Liberarus Sabas amesema mtuhumiwa mmojawapo Athumani Ramadhan Kassim alikamatwa baada ya taarifa za wasamari wema na kuwachukua polisi hadi eneo la ENGOSHERATON-SINON kwaajili ya kuwaonesha walipo wenzake, ndipo alipoanza kupaza sauti za “TAKBIR” na ghafla wenzake wakaanza kuwarushia polisi risasi.

Polisi wanasema baada ya upekuzi walikuta vifaa mbalimbali vya milipuko,kofia maalumu za kuficha uso (MASK),sare 5 za jeshi la wananchi (JWTZ),vaz moja la mchezo wa karete,pikipiki moja iliyobomolewa yenye namba bandia MC 983 BMK na bendera 2 nyeusi zenye maandishi ya kiarabu zinazotumiwa na makundi ya kigaidi.

Vitu vingine vilivyopatikana wakati wa upekuzi ni kisanduku cha chuma,hati ya kusafiria ya NDUGU Abrahaman Athuman Kangaa,simu tano za mkononi ambazo mojawapo ilitambuliwa kuwa ni ya marehemu Mary Joseph aliyefariki kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana mnamo tarehe 20/02/2016.

Adha Kamanda Sabas ameongeza kwamba katika eneo la tukio pia wamekuta,kifurushi cha unga wa baruti,kisu kimoja kikubwa,bunduki aina ya AK 47 na mafuta yake ya kusafishia pamoja na magazine yenye risasi 18 lakini pia karatasi yenye maneno ya vitisho kwa aliyekuwa kamanda wa kanda maalumu ya Dar es Salaam Suleiman Kova.

Kwa upande wa wakazi wa Arusha wametaka kuwemo na mkakati wa ziada kukabiliana na watu wahalifu wa aina hiyo kabla hawajaleta madhara.


Miili ya marehemu hao imehifadiwa katika hospitali ya mkoa ya Mount Meru kwaajili ya uchunguzi na utambuzi.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.