Breaking News
recent

Watu wasiofahamika wamembaka mtoto wa kike mwenye Umri wa miaka minne na nusu hadi kufa

Watu wasiofahamika wamembaka mtoto wa kike mwenye Umri wa miaka minne na nusu hadi kufa katika eneo la Makoko Manispaa ya Musoma Mkoani Mara na kisha kuutupa mwili wake.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo Kamishna Msaidizi Philip Kalangi amesema mtoto huyo alikua akisoma katika shule ya awali katika shule ya makoko katika Manispaa hiyo ambapo mwili wake ulikutwa katika jengo ambalo halijakamilika ujenzi wake.
                      Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo Kamishna Msaidizi Philip Kalangi 
Kamanda Kalangi amesema Polisi wanaendelea na kuwasaka watuhumiwa wa tukio hilo lakini amewataka wakazi wa maeneo hayo kukaa na kufikiria utaraibu wa kuwapeleka watoto wao shule iki kuepusha majanga kama hayo kuendelea kutokea.

Akizungumzia juu ya tukio hilo baba wa mtoto huyo amesema kuwa kawaida ya mtoto wao huwa anatoka shuleni kwa saa nane na kisha kurejea shule saa tisa jioni kwa ajili ya tuisheni lakini mama yake aliingiwa na wasiwasi baada ya mpaka saa moja usiku mtoto alikua hajarudi nyumbani na ndipo alipotoa taarifa na kuanza kumtafuta.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi ambae pia ni Mkuu wa Mkoa wa wilaya ya Musoma Zelothe Stephen amesema watu waliofanya kitendo hicho ni lazima wakamatwe huku akiwataka wazazi kuwa waangalifu jinsi ya kuwapeleka na kuwachukua watoto shuleni.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.