Breaking News
recent

YONO YAPEWA UDALALI WA KUWAFILISI WATEJA 24 WANAODAIWA ZAIDI BILIONI 18 BAADA YA KUTOROSHA MAKONTENA

Mamlaka ya Mapato nchini Tanzania(TRA), imeikabidhi Kampuni ya Udalali ya Yono uwafilisi wateja 24 wanaodaiwa kodi ya shilingi Bilioni 18.95 baada ya kutorosha makontena ya mizigo kwenye bandari kavu ya (ICD).

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Yono Kavela amesema hayo jana na kuongeza kuwa wameowa amari na TRA, ya kisheria ya kukamata mali za wadaiwa na kuwafilisi ili kulipa kodi wanazodaiwa.
          Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Yono Kavela
Bw, Kavela amesema baada ya kupata kazi hiyo wameona ni busara kutangaza na kuwapa siku 14 kulipa kodi wanazodaiwa na kwamba baada ya muda huo kumalizika hatua za kukamata mazli za wadaiwa zitaanza.

Majina ya wadaiwa hayo yametolewa jana kwa vyombo mbalimbali vya habari na kampuni hiyo ya udalali baada ya TRA, kuwakabidhi kazi ya kuwafilisi kutokana na kushindwa kutekeleza wajibu wao baada ya kupewa muda wa kufanya hivyo.


Kavela amesema ili kurahisha kazi Kampuni ya Said Salim Bakharesa ambayo ndio mmiliki wa bandari kavu pamoja na kampuni ya Regional Cargo Service wanapaswa kutoa ushirikiano kuhakikisha wadaiwa hao wanalipa kodi walizokwepa.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.