Breaking News
recent

Rais Magufuli amesema kuwa amepanga kupangua upya mishahara mikubwa ya wafanyakazi wanaopokea hadi shilingi milioni 40

Rais Magufuli amesema kuwa amepanga kupangua upya mishahara mikubwa ya wafanyakazi wanaopokea hadi shilingi milioni 40 na kusema kuwa lengo lake ni kuhakikisha katika kipindi chake kusikuwepo watu wanaolipwa zaidi ya shilingi milioni 15 kwa mwezi.

Ametolea mfano wa mfanyakazi mmoja wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) ambaye alikuwa akilipwa mishahara ya watu 17, na kueleza kuwa mfanyakazi huyo atafikishwa mahakamani.

Pia Rais Magufuli amesema serikali yake imejiandaa kuboresha maslai ya wafanyakazi kwa kupunguza kodi kutoka asilimia 11 ya sasa hadi asilimia 10 au 9 kuanzia bajeti ijayo,

Rais Magufuli amesema kwa wale wanaolipwa mishahara mikubwa ambayo inafikia hadi shilingi milioni 40, itapunguzwa na kuweka kima cha juu cha mshahara usiozidi shilingi milioni 15.

Kuhusu tatizo la wafanyakazi hewa, Rais Magufuli amesema uhakiki mdogo uliofanywa hivi karibuni, umebaini wafanyakazi hewa 1,680 waliokuwa wakilipwa shilingi bilioni 1 na milioni 800, na kwamba ni matarajio kuwa uhakiki unaofanywa nchi nzima utaisaidia serikali kubaini wafanyakazi hewa wengi zaidi na kunusuru fedha nyingi zaidi za watanzania.

Katika hatua nyingine Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametoa wito kwa kila mtanzania kuchapa kazi kwa juhudi ili nchi iondokane na utegemezi wa misaada ya wafadhili ambayo huambatana na masharti ambayo inawanufaisha zaidi wao.

Dkt. Magufuli amesema jukumu kubwa lililo mbele ya watanzania kwa sasa, ni kushikamana na kujisimamia katika maendeleo ili kila mmoja ahakikishe anaongeza uzalishaji na utendaji kazi mahali pake pa kazi.


Akizungumza na wananchi katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya sekondari Chato, Wilaya ya Chato Mkoani Geita Rais Magufuli amesema serikali yake imeamua kuchukua hatua kudhibiti nidhamu serikalini, kwa kuhakikisha inawachukulia hatua watumishi wa umma wanaolisababishia taifa upotevu mkubwa wa fedha, na ameahidi kuwa hatua hizo zitaendelea kuchukuliwa hadi tatizo hilo likomeshwe.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.