Breaking News
recent

Sakata la Kupigwa kwa Daktari Mkoani Mtwara, Ummy Mwalimu, amevitaka vyombo vya dola kutosita kuwachukulia hatua wananchi

Huduma za matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mtwara, Ligula, zilikosekana kwa muda baada ya madaktari na wauguzi wa hospitali hiyo kugoma kwa kushinikiza kutatuliwa kwa madai yao ikiwamo kuvitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuwatia nguvuni watu wanaodaiwa kumpiga daktari wa hospitali hiyo, dkt. Dickson Sahini.

Wakizungumza hospitalini hapo, baadhi ya wagonjwa wamesema kuwa toka wamewasili hakuna huduma yoyote ya matibabu iliyotolewa kwao zaidi ya kupokelewa mapokezi na kupatiwa cheti kisha kuambiwa wasubiri huku kukiwa hakuna dalili zozote za kuhudumiwa.

Wakizungumza mbele ya Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto, Mhe. Ummy Mwalimu, baadhi ya madaktari wa hospitali hiyo wamesema kuwa hali ya usalama wao iko mashakani kutokana na kutokuwapo kwa ulinzi wa kutosha hospitalini hapo huku wengine wakipata vitisho kutoka kwa wananchi.
                     Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto, Mhe. Ummy Mwalimu
Akitoa tamkoa la serikali juu ya tukio la kupigwa kwa daktari, Mhe. Ummy Mwalimu, amevitaka vyombo vya dola kutosita kuwachukulia hatua wananchi wote wanaokwenda kinyume na matakwa ya sheria ili kuwahakikishia watoa huduma za afya usalama na amani wakati wa kutekeleza wajibu wao.


Aidha, kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Henry Mwaibambe, amesema watuhumiwa wawili wanaodaiwa kutekeleza tukio hilo tayari wamekamatwa na wanatarajiwa kufikishwa mahakani haraka.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.