Breaking News
recent

Tanzania bado inakabiliwa na changamoto kuhakikisha kuwa kunakuwa na mazingira na ajira bora kwa watu wake

Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa - UNDP limetoa ripoti ya hali ya maendeleo ya mwanadamu kwa mwaka uliopita, inayoonyesha kuwa Tanzania bado inakabiliwa na changamoto kuhakikisha kuwa kunakuwa na mazingira na ajira bora kwa watu wake iwapo inataka kuboresha hali ya maisha kufikia dira ya taifa ya mwaka 2030.

Mwakilishi mkazi wa UNDP nchini Bw. Alvaro Rodrigues amesema kuna uhusiano wa karibu kati ya ajira bora na maendeleo ya watu hivyo kuna haja ya serikali kuwa na mipango inayotekelezeka ya kuboresha ajira na mazingira ya kazi kwa watu wake.
       Mwakilishi mkazi wa UNDP nchini Bw. Alvaro Rodrigues

Kwa upande wake, Waziri wa Kazi, Ajira, vijana na walemavu Anthony Mavunde amewataka waajiri kuheshimu sheria za kazi kwa kutoa mikataba ya ajira kwa wafanyakazi wao huku wakitambua kuwa amani na usalama ndio njia pekee inayoleta tija na ufanisi maeneo ya kazi.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.