Breaking News
recent

UTEUZI WA MKURUGENZI MPYA WA NSSF WATENGULIWA NDANI YA MASAA 24 BAADA YA KUTEULIWA

Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mheshimiwa Jenister Joakim Mhagama ametengua uteuzi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dkt. Carina Wangwe uliotangazwa leo Jijini Dar es salaam.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa usiku huu, imeeleza kuwa uteuzi huo umetenguliwa kutokana na kutokamilika kwa baadhi ya taratibu.
    ALIEKUA Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dkt. Carina Wangwe
Kulingana na Taarifa hiyo, uteuzi mpya kwa mujibu wa mamlaka na sheria utakapofanyika taarifa zitatolewa kwa wananchi.


Mapema Jana waziri Muhagama alimteua Dkt. Carina Wangwe kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Jamii(NSSF) kuchukua nfasi ya Mkurugenzi wa zamani Bw. Ramadhan Dau ambae aliteuliwa hivi karibu kuwa balozi.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.