Breaking News
recent

Magufuli akemea vitendo vya rushwa vinavyosababishwa ucheleweshwaji wa huduma ya usafirishaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amekemea vitendo vya rushwa vinavyosababishwa ucheleweshwaji wa huduma ya usafirishaji mipakani ikiwemo kwenye mipaka ya nchi ya Tanzania na Rwanda.

Akizungumza katika uzunduzi wa daraja la kimataifa la Rusumo linalounganisha Tanzania na Rwanda jana katika ziara yake ya kikazi aliyoianza nchini Rwanda rais Magufuli amesema kumekuwepo na vituo vya ukaguzi ambavyo lengo lake ni kuchukua rushwa.

Rais Magufuli amesema kuwa wingi wa vituo hivyo ulisababisha madereva kukaa muda mrefu njiani ikiwa ni zaidi ya wiki huku akisema kwa sasa anataka dereva asizidi siku tatu safari ya kutoka Dar es Salaam hadi Rwanda.

Ameongeza kuwa madereva wengi walikua wanachelewa kufika katika nchi hizo mbili kutokana na adham wanazozipata ikiwemo rushwa ambapo amesema wengi walikua wanatenga fedha za kutoa rushwa tangu mwanzo hadi mwisho wa Safari.


Kwa upande wake Rais wa Rwanda Paul Kagame amesema Ujenzi wa daraja hilo na kituo hicho utaimarisha uhisiano wa Tanzania na Rwada na amesema anategemea nchi hizo zitafanya kazi kwa pamoja kwa kukuza maendeleo endelevu
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.