Breaking News
recent

Arusha imeanza jitihada za kuwakamata watu wanaohusika na mtandao wa kuchoma moto shule za Bweni

Jeshi la Polisi Mkoani Arusha limeanza jitihada za kuwakamata watu wanaohusika na mtandao wa kuchoma moto shule za Bweni ,kufuatia mfululizo wa matukio ya shule za Bweni 6 kuteketezwa kwa moto siku za karibuni.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo, amesema kuwa majira ya saa 8 usiku tukio linguine la kuteketea kwa moto bweni la shule ya sekondari Winning Spirit mkoani Arusha limetokea ,chanzo cha moto huo bado hakijajulikana kwani uchunguzi unaendelea.
         Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo
Kamanda amesema kuwa tayari watumiwa 27 wanashikiliwa na jeshi hilo kwa kuhusishwa na matukio hayo ya moto na hatua zaidi zinachukuliwa kuhakikisha kuwa Wahusika wote wanabainiwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria..

Kamishna Msaidizi wa Jeshi la zima moto na Uokoaji mkoani Arusha Bakari Mrisho amesema kuwa kikosi chake kimefanya uchunguzi katika shule tano za bweni zilizoungua awali na kujirishisha kuwa ni hujuma za kibinadamu zimesababisha kuungua kwa mabweni hayo na kwasasa wamejielekeza kufanya ukaguzi katika shule za bweni na kuangalia iwapo zina uwezo wa kukabiliana na majanga ya moja.

Kwa upande wao wananchi wa Arusha Zakia Hassan na Patrick Samwel wameitaka serikali kuimarisha ulinzi katika shule za bweni ili kuepuka changamoto za mabweni kuungua moto.


Tayari shule sita mkoani Arusha zimekumbwa na janga la moto ikiwemo shule ya Sekondari Winning spirit,Lowasa sekondari,Nanja sekondari,Sokoine sekondari ,Longido sekondari pamoja shule ya sekondari Mlangarini.Juhudi za serikali na vyombo vyake zinahitajika kukomesha matukio hayo ya shule kuungua moto.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.