Breaking News
recent

CHADEMA),wameahirisha Maandamano ya kupinga kile wanachokiita wao ni Udikteta Uchwara (UKUTA)

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),wameahirisha Maandamano ya kupinga kile wanachokiita wao ni Udikteta Uchwara (UKUTA),ya nchi nzima ya kwa mwezi mmoja ili kutoa fursa ya viongozi wa dini na taasisi nyingine za amani na haki za binadamu kukaa na rais John Magufuli ili kulitatua suala hilo.

Akiongea kuhusiana na tamko hilo rasmi Mwenyekiti wa Chadema,Mhe. Freeman Mbowe amesema wamefikia hatua hiyo ya kuahirisha UKUTA lakini wamewataka wanachama wao kuendelea kusikiliza kauli za viongozi hao mpaka pale watakapo toa mwongozo mwingine kuhusiana na madai yao.
          Mwenyekiti wa Chadema,Mhe. Freeman Mbowe

Mbowe amesema licha ya Chadema kuwasikiliza Viongozi wa dini lakini CCM na serikali yao wao wamejipanga kufanya mapambano na viongozi wa Chadema na raia ambao wanataka kudai haki yao.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.