Breaking News
recent

HATUUNGI MKONO MAANDAMANO YOYOTE YA KISIASA-TUCTA

Shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini TUCTA, limesema kuwa haliungi mkono kusudio la baadhi ya vyama kufanya maandamano kinyume na utaratibu uliowekwa kisheria.

Katibu Mkuu wa TUCTA, Nicholaus Mgaya amewaambia waandishi wa habari mkoani Dodoma, amesema kuwa Shirikisho hilo limeundwa kwa ajili ya kutetea wafanyakazi na kamwe halijihusishi na masuala ya kisiasa.
              Katibu Mkuu wa TUCTA, Nicholaus Mgaya
Mgaya amesema kuwa Shirikisho hilo linaundwa na wajumbe wenye itikadi ya vyama tofauti lakini falsafa na sheria ya kuundwa kwa shirikisho hilo ni pamoja na kutojihusisha na masuala yoyote ya kisiasa kwa maslahi wa watu fulani.

Aidha Mgaya amesema licha ya kusimamia haki za kwa wafanyakazi lakini pia kusemea jamii kwa mambo ambayo hayaendi vizuri lakini pia kuishauri serikali ni jinsi gani ya kubana matumizi kwa ajili ya kujenga uchumi wa nchi kupitia wafanyakazi.


Katika hatua nyingine Mgaya amesema kuwa shirikisho hilo limepongeza hatua ya serikali kurudisha makao makuu ya nchi Mkoani Dodoma na kusema uamuzi huo utaotoa fursa kwa uchumi wa mkoa kukua kwa kasi.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.