Shirika
la kazi duniani ILO linakadiria kuwa ukosefu wa ajira kwa vijana
kimataifa utafifikia asilimia 13.1 mwaka huu wa 2016 na kusalia
katika kiwango hicho hadi mwaka 2017.
Ripoti ya Mtazamo wa kimataifa wa ajira na kijamii 2016 ikiwalenga
hasa vijana , inaonyesha kwamba idadi ya vijana wasiokuwa na ajira
itaongezeka kwa nusu milioni mwaka huu na kufikia milioni 71 kwa mara
ya kwanza katika kipindi cha miaka mitatu kushuhudia ongezeko hilo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Walemavu Jenista Mhagama
ILO
inasema cha kusikitisha zaidi ni idadi yay a vijana hasa katika nchi
zinazoendelea ambao wanaishi katika hali ya umasikini ama wa wastani
au wa kupindukia licha ya kuwa wanafanya kazi.
Takwimu
zinaonyesha kuwa vijana milioni 156 asilimia asilimia 33.7 wanao
fanya kazi wako katika hali ya umasikini ama wa wastani au wa
kupindukia ikilinganishwa na asilimia 26 ya watu wazima wanaofanya
kazi.

No comments:
Post a Comment