Breaking News
recent

MAHAKAMA KUREJESHA AMANI KWA WANANCHI KATIKA UTOAJI HAKI

Mahakama nchini Tanzania imejipanga kurejesha imani ya wananchi kwa mhimili huo muhimu katika utoaji wa haki kwa kuhakikisha uwazi na uwajibikaji pamoja na kupokea malalamiko ya wananchi na kuyapatia ufumbuzi kwa wakati.

Hayo yameelezwa Yameelezwa na Mtakwimu wa Mahakama ya Tanzania Idara ya Mipango na Ufuatiliaji Mcharo Mwanga na Naibu Msajili wa Mahakama ya Arusha Augustine Rwizile wakati wa kikao kazi cha kutoa elimu ya Mpango Mkakati wa Mahakama wa mwaka 2015/16-2019/2020.
   Mtakwimu wa Mahakama ya Tanzania Idara ya Mipango na Ufuatiliaji Mcharo Mwanga
Aidha wamesema kuwa Mpango huo utasaidia Mahakama kufanya kazi kwa ufanisi na kupokea mrejesho kutoka kwa wananchi kupitia Simu Maalumu za kupokea Malalamiko ya Wananchi juu ya uendeshaji wa shughuli za mahakama.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Jaji Fatuma Msengi amesema kuwa mpango mkakati huo utasaidia kuboresha mahusiano kati ya mahakama na wadau na pia kuwezesha upatikanaji wa haki kwa wakati


Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kwitega amesema kuwa suala la haki sawa na uwajibikaji wa mhimili wa Mahakama pamoja na uwazi litasaidia katika utendaji wa kila siku wa mahakama.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.