Breaking News
recent

SERIKALI YAAGIZA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA KUTATUA CHANGAMOTO YA UKOSEFU WA VYOO MASHULENI

Serikali imewaagiza wakuu wa mikoa na wilaya kuhakikisha inashirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ili kutatua changamoto ya ukosefu wa matundu ya vyoo iliyopo.

Naibu waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa SULEIMAN JAFO amesema hayo leo mjini Dodoma katika kikao cha kamati ya utawala na serikali za mitaa kwa ajili ya kutatua kero ya ukosefu wa madawati na miundombinu mingine katika sekta ya elimu.
Naibu waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa SULEIMAN JAFO 
Amesema jambo hilo ni la siku nyingi na linatia aibu na serikali peke yake haiwezi kukamilisha mahitaji yote ya matundu yaliyopo hivyo ni vyema wakuu hao wakashirikisha wadau ikiwemo nguvu kazi ya wananchi.

kwa upande wake mkurugenzi msimamizi wa elimu ofisi ya rais TAMISEMI JUMA KAPONDA amesema mahitaji ya matundu ya vyoo upande wa shule ya msingi ni 44,517 ambapo yaliyopo ni laki 162,754 na hivyo kuwepo wa upungufu wa matundu lajki 248,763.

Upande wa shule za sekondari mahitaji ni matundu elfu 42,365 wakati matundu yaliyopo ni 23,571 idadi ambayo inafanya uwepo wa upungufu wa matundu elfu 18,784.


KAPONDA amesema serikali kupitia bajeti yake ya mwaka 2016/2017 katika mapato ya ndani ya halmashauri imetenga jumkla ya shilingi bilioni 10.1 kwa ajili ya kujenga matundu ya vyoo elfu 8,791 katika shule za msingi na kwa shule za sekondari imetenga shilingi biliobi 2.5 kwa ajili ya ujenzi wa matundu elfu 1,942.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.