Breaking News
recent

WAZIRI MKUU AWATAKA VIJANA KWENDA SAMBAMBA NA KAULI MBIU YA HAPA KAZI TU ILI ILETE TIJA

Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amewataka vijana kuendana na kauli mbiu ya Serikali ya hapa Kazi tu ili iweze kuleta tija kutokana na Uchumi wa nchi unategemea zaidi mchango wa vijana katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Waziri Mkuu Majaliwa amesema hayo jana wakati akifungua Maonesho ya 24 ya wakulima maarufu kama nane nane kwa kanda ya Mashariki yaliyofanyika mkoani Morogoro katika viwanja vya mwalimu Julias Kambarage nyerere.
                Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa,
Mhe. Majaliwa amesema kuwa uchumi wa nchi unategemea zaidi kilimo hivyo amewataka vijana kujitokeza kwa wingi ili kuweza kufanya kilimo chenye tija kwao na taifa kwa ujumla na kufikia malengo yaliyowekwa na serikali.


Aidha Waziri Mkuu amesema kuwa kutokana na mkoa huo na matukio mengi ya migogoro ya wakulima na wafugaji serikali imeweka suluhisho ambalo litakua la kudumu ikiwemo kugawa vitalu kwa wakulima na wafigaji.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.