Breaking News
recent

Wafanyabishara katika standi ndogo ya Arusha wameandaman hadi ofisi za halmashauri

Wafanyabishara katika standi ndogo ya Arusha wameandaman hadi ofisi za halmashauri wakishinikiza kupewa mikataba ya maduka wanayopangisha wanayodai kuwa swala hilo limekuwa likipigwa danadana na ungozi wa jiji la Arusha.

Awali halmashauri ilitoa viwanja kwa wafanyabiashara ikiwataka kujenga na kutumia maduka hayo kwa kipindi cha miaka kumi bila kuilipa chochote, na baadae kukabidhi maduka hayo kwa halmashauri ya jiji..

Wafanyabiashara hao wameeleza kuwa sasa wamekuwa wakifanyabishara zao kwa wasiwasi, kufuatia mkanganyiko wa kimasilahi kati ya madalali wa maduka yao na halmashauri.

Kufuatia maelezo hayo Meya wa jijji la Arusha Kalisti Lazaro akalazimika kutoa maelelekezo ya namna yaulipaji huku akieleza kuwa tatizo kubwa ni madalali hao wamekuwa wakisababishia serikali upotevu wa mabilioni ya fedha kwa kutolipa mapato.
                          Meya wa jijji la Arusha Kalisti Lazaro 
Mstahiki meya amewataka wafanyabiashara hao kuendelea na majukumu yao huku akiwahakishia kuwa swala la mikataba linafanyiwa kazi katika kipindi kifupi .


Wakati mgogoro huo ukifukuta tayari duka moja limedaiwa kuvunjwa huku sababu kubwa ikidaiwa kuwa kushindwa kulipa kodi kwa halmashauri ,huku muhusika akidai amelipa kodi yake yote kwa mmilikiwa wa duka hilo.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.