Breaking News
recent

YALIYOJIRI KWA UFUPI KITAIFA NA KIMATAIFA

Kufuatia hatua ya Serikali kununua hisa zote za Bharti Airtel ambaye alikuwa mbia mwenza wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) na hivyo Serikali kumiliki hisa za Kampuni hiyo kwa asilimia 100, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemteua Bw. Waziri Waziri Kindamba kuwa Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL.

Bw. Waziri Waziri Kindamba ameteuliwa kushika nafasi hiyo kuanzia leo tarehe 23 Septemba, 2016 huku aliyekuwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Dkt. Kamugisha Kazaura atapangiwa kazi nyingine.
………………………………...
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Watoto nchini Tanzania (UNICEF) na serikali wamezindua hatua mpya ya usajili wa watoto wote wanaozaliwa na walio na umri wa chini ya miaka mitano mradi huo ulioanza mwaka 2012 kwa majaribio una lengo la kufikia mikoa yote ya Tanzania.

Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni hiyo Waziri wa Katiba na Sheria Dk. Harrison Mwakyembe amesema hadi sasa watoto 400,000 wameshasajiliwa na kupewa vyeti vya kuzaliwa katika mikoa ya Mbeya na Mwanza na sasa kampeni hiyo imeingia mikoa ya Iringa na Njombe.
………………………………....

Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), leo limezindua mkakati wa kukabiliana na magonjwa ya moyo yakiwamo shambulio la moyo na kiharusi, magonjwa yanayoongoza kwa kusababisha vifo duniani.

Kwa mujibu wa WHO, zaidi ya watu milioni 17 hufariki dunia kila mwaka kutokana na magonjwa ya moyo, wengi wa wanaofariki hugundulika kutumia tumbaku, kula vyakula vyenye chumvi nyingi, na kutofanya mazoezi ambapo shirika hilo limesema wengi wanaweza kuokolewa kwa kupatiwa tiba mbalimbali.
.. .................................................
Maafisa polisi wawili wameripotiwa kutojulikana walipo baada wapiganaji wa Al-Shabaab kushambulia kambi yao ya Hamey katika kaunti ya Garissa nchini Kenya.

Msemaji wa jeshi la polisi Kenya, George Kinoti amesema washambualiaji hao wameiba bunduki aina ya machine gun, risasi 1,000 pamoja gari aina ya Toyota Land cruiser.
..............................................

Manusura wa bodi iliyozama kwenye eneo la karibu na Pwani ya Misri, wamesema kuwa mamia ya watu huenda wamekufa maji.

Boti lililozama lilikuwa limebeba kati ya watu 450 ama 600 ambao ni wahamiaji ilipozama kilomita 12 kutoka ufukwe wa Misri.
…………………….................
Na,
Utafiti uliofanywa nchini Uingereza umebaini kuwa wanawake wengi wanofanyakazi wamekuwa wakipata maumivu ya makali wakati wa hedhi, ambayo yamekuwa yakiathiri uwezo wao wa kufanyakazi.


Utafiti huo uliofanywa kwa wanawake 1,000 umebaini kuwa asilimia 52 kati yao hupatwa na maumivu makali ya hedhi, lakini ni asilimia 27 tu walioweza kuwaambia mabosi wao kuwa ufanisi wao umeathiriwa na maumivu hayo.
                                       Goza News
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.