Breaking News
recent

WALIMU SITA WANASHIKILIWA NA POLISI NJOMBE KWA KUMPIGA MWANAFUNZI HADI KUZIMIA KWA KOSA LA KUKUTWA NA SIMU KWENYE TRANKA LAKE

Siku chache baada ya kutokea tukio la kushambuliwa mwanafunzi ikiwa kama adhabu mkoani Mbeya, waalimu sita wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Njombe baada ya kudaiwa kumshambulia mwanafunzi wa kike wa kidato cha nne kwa kosa la kukutwa simu ya mkononi katika begi lake la chuma la nguo na waalimu wake.

Mwanafunzi huyo wa shule ya binafsi ya sekondari ya Mbogamo, ya mkoani Njombe, Elizabeth Simfukwe anadaiwa kushambuliwa na mkuu wa shule akiwa na waalimu wengine na kumsababishia maumivu kisha kulazwa katika Hospitali ya Kibena mkoani Njombe kwa siku zaidi ya tatu akipatiwa matibabu mzazi wake.
          Wanafunzi wakiwa nje ya shule yao ya Mbogamo Commerce Secondary School
Baada ya mwandishi wa habari kufika katika Hospitali ya kibena ya mkoani Njombe ambapo mwanafunzi mwanafunzi huyo amelazwa,Uongozi wa Hospital hiyo umesema kuwa umezuiliwa kuzungumzia taarifa hiyo kutokana na suala hilo lipo chini ya vyombo vya usalama.

Mkuu wa wilaya ya Njombe Ruth Msafiri akiongea na East Afrika Radio kwa njia ya simu amekiri kutokea kwa tukio hilo wilayani kwake licha ya yeye kuwa mbali ofisi amesema ni kweli mwanafunzi huyo alikutwa na kosa lakini sheria iliyotumika kumuadhibu ni kinyume cha sheria zilizowekwa na serikali.


Kituo hiki kilifika shuleni hapo na kubaini kutokuwepo kwa walimu hao na kuthibitika kuwa wanashikiliwa na vyombo vya usalama huku shule hiyoi ikiwabakiwa na mwalimu mmoja tu kutokana na tukio hilo.
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.