Breaking News
recent

Serikali imesema hali ya upatikanaji wa dawa nchini imeiimarika

Serikali imesema kuwa hali ya upatikanaji wa dawa nchini imeiimarika hadi kufikia asilimia 80 ikiwa ni kutokana na ongezeko la fedha zilizopelekwa Bohari Kuu ya Dawa, (MSD), ili kuviwezesha vituo vya afya vya umma nchini kupata mahitaji yake ya dawa, vifaa tiba na vitendanishi.
Akizungumza leo Bungeni Mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamis Kingwangalla amesema hali hiyo imetokana na serikali kuongeza bajeti dawa kutoka shilingi bilioni 31 hadi kufikia bilioni 251.5 katika mwaka wa fedha 2016/2017.
Dkt. Kigwangala amesema kuwa changamoto iliyokuwepo hapo awaloi ni kutokana na mfumo uliokua unatumika katika usambazaji kukumbwa na changamoto ya ukosefu wa fedha lakini kwa sasa tatizo hilo linaelekea kumalizika kutokana na kuongezewa bajeti ya dawa kwa wizara.
Aidha Naibu Waziri huyo amewataka wabunge na viongozi wengine kushirikiana na Wizara hiyo katika kupata taarifa juu ya wizi wa dawa katika vituo vya afya kutokana na mfumo uliopo sasa kutoka mianya ya wizi huo wa dawa katika maeneo mbalimbali nchini.

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamis Kingwangalla 
gmbongo tha entertainer

gmbongo tha entertainer

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.